Orodha mpya ya mabilionea Afrika yamshirikisha Dangote , Mo Dewji na Isabel dos Santos
Abdalla Seif Dzungu
BBC Swahili
18 Januari 2020
Aliko Dangote
CHANZO CHA PICHA,AFP
Maelezo ya picha,
Mtu tajiri zaidi barani Afrika Aliko Dangote
Mfanyabiashara Mohammed Dewji kutoka Tanzania ametajwa kuwa miongoni mwa mabilioni 20 wa Afrika katika ripoti ya jarida la Forbes la mwaka 2020.
Hatahivyo utajiri wa bilionea wa Tanzania Mo umedaiwa kupungua hadi dola bilioni 1.6.
Katika ripoti hiyo mfanyabiashara tajiri nchini Nigeria Aliko Dangote ameorodheshwa kwa mara ya tisa mfululizo, kuwa mtu tajiri zaidi barani Afrika .
Dangote mwenye umri wa miaka 62 ambaye anafanya biashara ya Simiti, Sukari na unga wa ngano ana utajiri wa dola Bilioni 10.1.
Pia unaweza kusoma:
Vijana walio tajiri zaidi duniani
Watu wanane matajiri kupindukia duniani
Dangote anafuatiwa na mfanyabiashara wa Misri Nassef Sawaris ambaye aliongeza utajiri wake kutoka dola bilioni 6.3 hadi dola bilioni nane.
Mfanyabiashara huyo anamiliki asilimia 5.7 ya hisa za kamapuni ya viatu ya Adidas . Ongezeko la hisa za Adidas liliomuongezea dola bilioni moja nukta tano katika akaunti yake.
Mo Dewji
CHANZO CHA PICHA,HAKI MILIKI YA PICHAAFP/GETTY IMAGES
Maelezo ya picha,
Bilionea kutoka Tanzania Mo Dewji
Bilionea aliyeorodheshwa katika nafasi ya tatu ni raia wa Nigeria Mike Adenuga ambaye utajiri wake unatokana na sekta ya mawasiliano na mafuta. Kampuni yake ya mawasiliano ya simu Globacom ndio ya tatu kwa ukubwa nchini Nigeria ikiwa na wateja milioni 43.
Alijipatia utajiri wake wa kwanza akiwa na umri wa miaka 26 akiuza kanda za viatu na vinywaji.
Bilionea aliyeorodheshwa wa nne barani Afrika ni mfanyabiashara wa almasi na raia wa Afrika Kusini Nicky Oppenheimer.
Nicky ambaye ni mrithi wa mali ya familia yake ya Oppenheimer ana utajiri wa dola bilioni 7.7.
Familia yake imekuwa ikihusika na uuzaji wa almasi.
Isabel dos Santos mwenye utajiri wa dola bilioni 2.2 amedaiwa kujipatia utajiri wake wakati babake alipokuwa rais ambapo alijipatia hisa katika makampuni mengi ya Angola pamoja na benki.
Mwanamke huyo ambaye ametajwa kuwa mwanamke tajiri zaidi barani Afrika amesema kwamba anamiliki hisa kutoka kampuni zilizopo Ureno, ikiwemo Telecom na runinga ya nyaya.
Msemaji wa Isabel aliambia jarida la Forbes kwamba ni mfanyabiashara huru .
Isabel dos Santos
Comments